Bashe Akabidhi Magari Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama Vya Ushirika (COASCO)

Bashe Akabidhi Magari Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama Vya Ushirika (COASCO)

Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama Vya Ushirika (COASCO) limekabidhiwa magari matano ili liweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi.

Magari hayo ni kati ya 38 yaliyokabidhiwa na Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe kwenye Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo pamoja na mitambo ya uchimbaji visima, itakayotumika katika shughuli za wizara na Taasisi zake za umwagiliaji.

Akikabidhi magari hayo kwa shirika hilo, Waziri Bashe amesema wameanza kuisaidia COASCO ili iweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi.

“Angalau tumeanza kuisaidia COASCO ili iweze kutimiza wajibu wake. Tunaamini utendaji wa COASCO kwani sasa hivi wana rasilimali za kibajeti wameanza kupata, vitendea kazi wameanza kupata ili waweze kutimiza wajibu na kuonesha thamani ya fedha na naamini maono ya COASCO yatabadilika.” Alisema Bashe.

Aidha, alisema wizara yake inatarajia kuanzisha mpango wa ruzuku ya uchimbaji visima kwa ajili ya wakulima wa kipato cha chini, ambapo visima vitachimbwa bila malipo.

Related Articles

Visitor Counter

000727
Today: 8
Yesterday: 4
This Week: 8
Last Week: 91
This Month: 210

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz