Waziri Mkuu Aridhishwa na Maandalizi Kuelekea Sherehe za Mei Mosi

Waziri Mkuu Aridhishwa na Maandalizi Kuelekea Sherehe za Mei Mosi


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema ameridhishwa na Maandalizi kuelekea sherehe za siku ya wafanyakazi Duniani zitakazofanyika kesho Mei mosi, 2025 kitaifa Mkoani Singida katika Uwanja wa Bombadia
 
Ameyasema hayo leo Jumatano Aprili 30, 2025 alipopokea taarifa na kukagua maandalizi ya Maadhimisho ya Sherehe hizo ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Majaliwa ameipongeza kamati inayoratibu sherehe hizo na kuwataka kuhakikisha wanakamilisha maeneo machache yaliyobaki ambayo yanahitaji maboresho.
 
Awali, akitoa taarifa ya maandalizi hayo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Ridhiwani Kikwete amesema maandalizi yamekamilika kwa kiasi kikubwa na wapo tayari kumpokea Rais Dkt. Samia kwa ajili ya sherehe hizo.

DC Shaka Ahimiza Suala la Lishe Mashuleni Ataka Walimu,wazazi na Watendaji wa Kata Kujitoa

DC Shaka Ahimiza Suala la Lishe Mashuleni Ataka Walimu,wazazi na Watendaji wa Kata Kujitoa

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa  Shaka Hamdu Shaka, ametoa wito kwa wazazi, walimu, na watendaji wa kata kushirikiana kwa karibu katika kuhakikisha wanafunzi wanapata chakula cha mchana shuleni.

Amesisitiza kuwa lishe bora ni msingi wa maendeleo ya elimu na afya kwa watoto, hivyo ni jukumu la kila mmoja katika jamii kuhakikisha suala hilo linapewa kipaumbele na kwamba hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa kila shule ina uwezo wa kuzalisha chakula chake, hivyo kuboresha lishe ya wanafunzi na kuongeza ufanisi katika elimu.

Shaka amebainisha kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa imejipanga kutumia rasilimali zilizopo, hususani ardhi yenye rutuba, kwa ajili ya kilimo cha chakula cha shule ambapo ametoa rai kwa watendaji wa kata ambao hawana maeneo ya kilimo kutoa taarifa ili wapatiwe ardhi kwa ajili ya shughuli hiyo muhimu.


Kikao hicho kimewashirikisha watendaji wa kata zote 40 pamoja na wataalam mbalimbali wa sekta ya lishe na elimu, DC Shaka amewataka watendaji hao kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake kuweka mkazo katika suala la lishe kwa wanafunzi huku akisisitiza kuwa agizo la kuhakikisha lishe bora kwa wanafunzi ni maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, hivyo ni lazima litekelezwe kwa vitendo.

Katika hatua nyingine DC  Shaka ameahidi kuwa wilaya ya Kilosa itaendelea kumuunga mkono  Rais kwa kuhakikisha kuwa suala la lishe kwa wanafunzi linapewa kipaumbele cha juu nakusema kuwa kwa kushirikiana na wazazi, walimu, na watendaji wa kata, watahakikisha kuwa kila mwanafunzi anapata chakula cha mchana shuleni, hivyo kuboresha afya na ufaulu wao.
Serikali Kujenga Vituo Sita vya Forodha Mwaka wa Fedha 2025/2026

Serikali Kujenga Vituo Sita vya Forodha Mwaka wa Fedha 2025/2026

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesema kuwa ina mpango wa kujenga vituo sita vya forodha mipakani katika mwaka wa fedha ujao wa 2025/26.

Hayo yamesemwa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Hamad Hassan Chande (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Oliver Daniel Semuguruka, aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kuanza ujenzi wa Kituo cha Forodha katika Kijiji cha Mukikoro, Kata ya Mugoma - Ngara.

Chande alisema kuwa Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 1.1 ya ujenzi wa vituo Sita vya forodha kikiwemo kituo cha forodha Mugoma kilichopo Wilaya ya Ngara, mkoani Kagera mpakani mwa Tanzania na Burundi kwa mwaka ujao wa fedha.

 

CHADEMA Yalaani Uvamizi wa Makazi ya Viongozi Wao

CHADEMA Yalaani Uvamizi wa Makazi ya Viongozi Wao

Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA kimedai Jeshi la Polisi kuendesha operesheni haramu ya kuzingira na kuvamia makazi ya viongozi wa chama hicho ambao ni Mwenyekiti wa Chama Mh. Tundu Lissu na Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho. Mh. John Heche

Kwa mujibu wa Taarifa iliyo na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi Bi. Brandina Rupia imeeleza kuwa Katika makazi ya Mhe. Tundu Lissu, Askari wa Jeshi la Polisi wamevamia makazi ya Mh Lisu wakitaka kufanya upekuzi wa nyumba (upekuzi usiofuata sheria na taratibu), huku wakitumia lugha za vitisho na vitendo vinavyokiuka misingi ya kisheria na haki za binadamu.

Aidha taarifa hiyo imepinga kwa nguvu zote uvunjaji huo wa sheria na taratibu na kutaka majibu ya haraka kwa maswali sita waliouliza Jeshi la Polisi na Serikali ya CCM:

1. Kwa nini walitaka kufanya upekuzi usiku wa manane kama majambazi badala ya mchana kwa uwazi na kufuata taratibu na sheria?

2. Kwa nini hawakuonesha hati halali ya upekuzi kutoka mahakamani (Search Warrant) kama sheria inavyotaka?

3.Kwa nini hawakuambatana na kiongozi wa mtaa ili kushuhudia upekuzi kama taratibu na sheria zinavyowataka?

4. Kwa nini mnapanga kutekeleza au kufanya upekuzi katika nyumba ambayo mmiliki wake yupo gerezani na hawezi kushuhudia?

5. Je, Jeshi la Polisi linakusudia kumuweka Mhe. John Heche chini ya kifungo

GASCO kutumia Vifaa vya Kisasa Kuhakikisha usalama na Afya bora  kwa Wafanyakazi

GASCO kutumia Vifaa vya Kisasa Kuhakikisha usalama na Afya bora kwa Wafanyakazi

Kampuni ya Gesi Tanzania (GASCO) ambayo ni kampuni tanzu ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) imesema kuwa imewekeza vya kutosha katika matumizi ya teknolojia inayotumia akili mnemba (AI) kwa ajili ya kulinda usalama wa watu au wafanyakazi na mitambo ya kuchakata kusafirisha na usambazaji gesi asilia . 
 
Akizungumza wakati wa Maonesho ya Maadhimisho ya Wiki ya Usalama na Afya Mahala Pa Kazi Duniani yanayofanyika Kitaifa mkoani Singida, Afisa Usalama na Mazingira Mahala Pa Kazi wa GASCO Bw. Mlotwa Simbeye amesema kuwa shughuli za gesi asilia zinahitaji umakini mkubwa wa usalama na ndio maana wanatumia mifumo ya kisasa ya utambuzi na ung’amuzi wa vihatarishi mbalimbali kama vile gesi kuvuja au majanga ya moto ili kuzuia madhara yanayoweza kutokea.
 
Akiongea katika maonesho hayo, Mhandisi Hassan Temba amesema GASCO ina jukumu kubwa la usimamizi, uendeshaji na matenegezo ya mitambo ya Uchakataji, Usafirishaji na Usambazaji Gesi Asilia hapa nchini.
 
Pia, inahusika na ujenzi wa miundombinu ya gesi asilia ikiwemo ujenzi wa bomba la usambazaji wa gesi kwa wateja wa viwandani na majumbani pamoja na ujenzi wa vituo vya mafuta na gesi asilia kwenye magari (CNG)
 
“Ndio maana tumeamua kushiriki maonesho haya ili Watanzania waweze kujua kazi za GASCO kwa maendeleo ya nchi,” amesema Temba.
 
Aidha, Afisa Maendeleo ya jamii wa TPDC Bw.Oscar Mwakasege amesema kuwa TPDC ina majukumu mbalimbali ikiwemo kusimamia miradi ya kimkakati ya utafiti na utafutaji wa mafuta na gesi asilia nchini ukiwemo mradi wa utafiti wa mafuta Kitalu cha Eyasi Wembere ambao unagusa mikoa mitano (5) ikiwemo mkoa wa Singida (Wilaya ya Iramba na Mkalama).
 
‘‘Vilevile, TPDC ni mdau mkubwa wa maendeleo ya jamii kwani kupitia programu ya CSR miradi mbalimbali imetekelezwa ili kuleta ustawi wa na kudumisha mahusiano na jamii zinazopitiwa na miradi ya gesi asilia nchini. Mkoani Mtwara TPDC imekamilisha ujenzi wa kituo cha afya cha Msimbati mkoani Mtwara’’. Amesema Oscar
 
Kauli mbiu ya maonesho hayo yaliyoandaliwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) ni ‘Nafasi ya Akili Mnemba na Teknolojia za Kidijitali katika Kuimarisha Usalama na Afya Mahali pa Kazi’ ambapo mashirika na makampuni mbalimbali yameshiriki na kuonyesha mifumo yao ya afya na usalama kazini.

Visitor Counter

000531
Today: 5
Yesterday: 9
This Week: 41
Last Week: 32
This Month: 14

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz