Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA kimedai Jeshi la Polisi kuendesha operesheni haramu ya kuzingira na kuvamia makazi ya viongozi wa chama hicho ambao ni Mwenyekiti wa Chama Mh. Tundu Lissu na Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho. Mh. John Heche
Kwa mujibu wa Taarifa iliyo na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi Bi. Brandina Rupia imeeleza kuwa Katika makazi ya Mhe. Tundu Lissu, Askari wa Jeshi la Polisi wamevamia makazi ya Mh Lisu wakitaka kufanya upekuzi wa nyumba (upekuzi usiofuata sheria na taratibu), huku wakitumia lugha za vitisho na vitendo vinavyokiuka misingi ya kisheria na haki za binadamu.
Aidha taarifa hiyo imepinga kwa nguvu zote uvunjaji huo wa sheria na taratibu na kutaka majibu ya haraka kwa maswali sita waliouliza Jeshi la Polisi na Serikali ya CCM:
1. Kwa nini walitaka kufanya upekuzi usiku wa manane kama majambazi badala ya mchana kwa uwazi na kufuata taratibu na sheria?
2. Kwa nini hawakuonesha hati halali ya upekuzi kutoka mahakamani (Search Warrant) kama sheria inavyotaka?
3.Kwa nini hawakuambatana na kiongozi wa mtaa ili kushuhudia upekuzi kama taratibu na sheria zinavyowataka?
4. Kwa nini mnapanga kutekeleza au kufanya upekuzi katika nyumba ambayo mmiliki wake yupo gerezani na hawezi kushuhudia?
5. Je, Jeshi la Polisi linakusudia kumuweka Mhe. John Heche chini ya kifungo
