Dkt. Nchimbi awahasa waandishi wa habari kutumia kalamu zao kuimarisha  amani katika jamii.

Dkt. Nchimbi awahasa waandishi wa habari kutumia kalamu zao kuimarisha amani katika jamii.

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi , Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, amewataka wahariri wa vyombo vya habari pamoja na waandishi wa habari kuzitumia kalamu zao vizuri ili kuchochea amani, utulivu, na kuongeza umoja katika jamii, badala ya kuzusha vurugu.

Ametoa wito huo April 04,2025  mjini Songea, mkoani Ruvuma katika Mkutano mkuu Maalum wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), kuelekea uchaguzi wa viongozi wa jukwaa hilo, unaofanyika leo  Aprili 5, 2025, wenye lengo la kumpata  Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, na wajumbe wa Kamati ya Utendaji wa jukwaa hilo.

Balozi Nchimbi amepongeza kazi kubwa zinazofanywa na wahariri katika kuzitangaza 4R za Rais Samia Suluhu Hassan, ambazo sasa jamii imeanza kuzielewa na kusema ni dhahiri kwamba wananchi wanatambua umuhimu wa vyombo vya habari. Ameiomba TEF kuendelea kufanya kazi ya kujenga jamii ya Tanzania.

Aidha, amewapongeza wahariri kwa kuwa chujio la habari zote katika Taifa, akieleza kuwa endapo wangetumia nafasi zao vibaya, jamii ingekuwa katika hali tofauti na ilivyo sasa.

Balozi Nchimbi alibainisha kuwa Chama cha Mapinduzi kinatambua mchango mkubwa wa vyombo vya habari na dhamira ya chama hicho ni kuhakikisha vyombo hivyo vinafanya kazi kwa uhuru huku akibainisha  kuwa katika kipindi cha miaka mitatu, Tanzania imepiga hatua kubwa, ikiwa imezipita nchi zaidi ya 50  kwa kuwa na uhuru wa vyombo vya habari.

Related Articles

Visitor Counter

000531
Today: 5
Yesterday: 9
This Week: 41
Last Week: 32
This Month: 14

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz