Friedrich Merz Kurithi  Kiti cha  Ukansela wa Ujerumani

Friedrich Merz Kurithi Kiti cha Ukansela wa Ujerumani

Mwanasiasa wa kihafidhina kutoka muungano wa vyama ndugu vya CDU/CSU, Friedrich Merz, anatarajiwa leo kuchaguliwa na Bunge kuwa Kansela mpya wa Ujerumani

Hatua hiyo inajiri zaidi ya miezi miwili tangu ulipofanyika uchaguzi mwishoni mwa mwezi Februari.

Merz ambaye alikuwa mgombea wa vyama hivyo viwili vilivyopata ushindi mwembamba kwenye uchaguzi huo, atachukua rasmi wadhifa wa ukansela pale bunge la taifa, Bundestag, litakapopiga kura mjini Berlin ili kumuidhinisha.

Ataongoza serikali ya mseto na chama cha siasa za wastani za mrengo wa kushoto cha SPD, ambacho ni cha kansela anayeondoka, Olaf Scholz.

Akizungumza baada ya kutia saini makubaliano ya kuunda serikali, Merz amesema anatumai watamudu kuiongoza Ujerumani kwa njia madhubuti na kushughulikia changamoto zinazolikabili taifa hilo lenye uchumi mkubwa zaidi barani Ulaya.

 
 

Related Articles

Visitor Counter

000970
Today: 1
Yesterday: 14
This Week: 18
Last Week: 49
This Month: 122

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz