Rais Donald Trump Amteua Waltz Kuwa Balozi  UN

Rais Donald Trump Amteua Waltz Kuwa Balozi UN

Rais Donald Trump ametangaza  kumteua mshauri wake wa usalama wa kitaifa, Mike Waltz, kuwa balozi wa Marekani katika Shirika la Umoja wa Mataifa.

Trump ametoa tangazo hilo Mei mosi 2025,  kupitia mtandao wake wa kijamii wa Truth Social  huku  Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio  akatarajiwa kushika nafasi ya Mike Waltz kwa muda.

Tangazo hilo lilitolewa saa chache kufuatia ripoti kuwa  Waltz na naibu wake, Alex Wong, watajiuzulu nafasi zao, wakati shinikizo likizidi kuhusu jukumu la Waltz kwenye kashfa ya Signalgate.

Waltz alimuunga bila kukusudia mwandishi wa habari kwenye kundi ambalo hujadiliana taarifa za siri hususani za mipango ya vita, hatua iliyobua madai ya taarifa hizo kuvuja

Katibu Mkuu wa UN Ahimiza Juhudi Kumaliza Mgogoro Mashariki ya Kati.

Katibu Mkuu wa UN Ahimiza Juhudi Kumaliza Mgogoro Mashariki ya Kati.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametahadharisha kuwa eneo la Mashariki ya Kati lipo katika njia panda kuhusu ahadi ya suluhisho la mataifa mawili katika mzozo kati ya Israel na mamlaka ya Palestina.

Guterres ameliambia baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kwamba ahadi hiyo ya suluhisho la mataifa mawili iko hatarini kutoweka kabisa na kuongeza kuwa utashi wa kisiasa wa kufanikisha lengo hilo unaonekana kuwa mbali zaidi sasa kuliko wakati wowote ule.

"Muda unakwenda suluhisho la mataifa mawili liko karibu kufikia hatua isiyoweza kurudi nyuma Jamii ya kimataifa ina jukumu la kuzuia ukaliaji wa kudumu na vurugu." amasema  Guterres

Katibu Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa amehimiza mataifa kuchukua hatua zaidi na si kutoa kauli  pekee na kueleza hatua mahususi za kufufua suluhisho la mataifa  hayo mawili.

Amesema ana wasiwasi mkubwa kuhusu kuzorota kwa hali ya kibinadamu katika ukanda wa Gaza ambapo takribani  Wapalestina 2,000 wameuawa tangu makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyofikiwa mwezi Machi yaliposambaratika.

 

 

Kesi ya Mwanamke Anayeshutumiwa Kumuua Ndugu  yake Kwa Uyoga Wenye Sumu Yaanza Kusikilizwa

Kesi ya Mwanamke Anayeshutumiwa Kumuua Ndugu yake Kwa Uyoga Wenye Sumu Yaanza Kusikilizwa

Kesi ya mwanamke mmoja  anayafahamika kwa jina la Erin Patterson (50)  amabaye anashutumiwa  kwa kuwauwa ndugu zake  kwa uyoga wenye sumu wakati wa chakula cha mchana imeanza kusikilizwa ambapo mwanamke huyo  anakabiliwa na mashtaka matatu ya mauaji shtaka moja likiwa ni kujaribu kuua   kwa chakula cha mchana chenye sumu  alichowapa  ndugu zake  huko Gippsland Kusini mnamo mwaka 2023.

 Mahakama imesema kuwa Polisi hawajawahi kupata simu iliyotumika na Erin Patterson siku hiyo na simu nyingine iliyopatikana na kuchukuliwa wakati wanafanya msako nyumbani kwake ilikuwa imefutwa kila kitu na kurejeshwa ilivyokuwa mwanzoni.

Patterson pia aliwaambia polisi hajawahi kuwa na chombo cha kukausha chakula licha ya CCTV kumwonyesha akitupa kifaa hicho, na utafiti wa ujasusi baadaye ukaonyesha kuwa kifaa hicho kina alama za vidole vyake na kilipatikana na mabaki ya uyoga wenye sumu.

 

Mume wa mwimbaji wa Muziki wa Injili  Nigeria Aukumiwa  kunyongwa hadi Kufa

Mume wa mwimbaji wa Muziki wa Injili Nigeria Aukumiwa kunyongwa hadi Kufa

Mahakama kuu huko Abuja nchini Nigeria  imemhukumu Peter Nwachukwu, mume wa mwimbaji maarufu wa injili Osinachi, adhabu ya kunyongwa hadi kifo  baada ya  kupatikana na hatia ya mauaji.

Hukumu hiyo, iliyotolewa na jaji Nwosu-Iheme, imetolewa miaka mitatu baada ya kifo cha osinachi kilichotokea mnamo aprili 8, 2022. Kesi hiyo imejulikana zaidi  kwa sababu ya umaarufu wa Osinachi katika muziki wa injili wa Nigeria na jamii ya wakristo.

Polisi walikuwa wamemkamata bwana nwachukwu baada ya mkewe, kufariki akiwa katika hospitali moja huko Abuja  huku ripoti za awali zikiwa zimependekeza kuwa  mwanamke huyo aliyekuwa na umri wa miaka 42 alikuwa mgonjwa wa saratani ya koo, lakini familia yake ilikataa na kudai kwamba alikuwa mwathirika wa unyanyasaji wa nyumbani.

Chama cha Waziri Mkuu  wa Canada chashinda Uchaguzi

Chama cha Waziri Mkuu wa Canada chashinda Uchaguzi

Matokeo ya awali yanaonyesha kuwa Chama cha kiliberali cha Waziri Mkuu wa Canada Mark Carney kimeshinda uchaguzi wa Bunge na hivyo kujipatia muhula mwengine madarakani.

Lakini haijawa wazi ikiwa chama hicho kitapata idadi kubwa ya wabunge na kukipiku chama cha wahafidhina kinachoongozwa na Pierre Poilievre. Canada imefanya uchaguzi wake wa bunge Aprili 28, 2025  ili kuamua chama kitakachoiongoza Serikali ijayo chini ya kiwingu cha mivutano na Taifa jirani na lenye nguvu za kiuchumi Marekani.  Wapiga kura walikuwa wanaamua kati ya kukirejesha madarakani chama cha Kiliberali chini ya mwanasiasa  Mark Carney  au kuwachagua wahafidhina wanaoongozwa na mwanasiasa Pierre Poilierve .

Zaidi ya raia milioni 28  wa Canada waliorodeshwa kwenye daftari la wapiga kura. Uchaguzi huu ulishuhudia pia rekodi ya raia milioni 7.3 waliofanikiwa kupiga kura ya mapema. Baadhi ya vituo vya kupigia kura vilifungwa usiku wa jana na kura kuanza kuhesabiwa.

Pia, uchaguzi huo ulionekana kuwa muhimu kwa rais wa Marekani Donald Trump ambaye kama kawaida yake aliandika kwenye mitandao ya kijamii na kuwatolea wito raia wa Canada kumchagua kiongozi ambaye atakuwa na busara na ujasiri wa kuifanya nchi hiyo kuwa jimbo la 51 la Marekani akidai kuwa itakuwa fursa kubwa kwa Canada.

Hata hivyo, wakati wa kampeni, wagombea wakuu katika uchaguzi huo ambao ni Mark Carney wa chama cha Kiliberali na mhafidhina Pierre Poilierve hawakuzungumzia suala hilo la Canada kuwa jimbo la Marekani, fikra ambayo hata hivyo inapingwa vikali na idadi kubwa ya raia wa nchi hiyo.

Visitor Counter

000531
Today: 5
Yesterday: 9
This Week: 41
Last Week: 32
This Month: 14

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz