Iran Yatangaza Vifo vya Majenerali Sita, Yumo Mkuu wa kikosi cha Walinzi wa Mapinduzi

Iran Yatangaza Vifo vya Majenerali Sita, Yumo Mkuu wa kikosi cha Walinzi wa Mapinduzi

Kikosi Maalum cha Walinzi wa Mapinduzi nchini Iran, kimetangaza vifo vya majenerali sita hali iliyoongeza idadi ya maafisa wakuu waliouawa katika kampeni ya kijeshi ya Israel kufikia  watu wapatao16.

kwa mujibu wa shirika la habari la Tasnim lenye ushirikiano wa karibu na kikosi hicho cha Walinzi wa Mapinduzi, mazishi ya Salami, Bagheri na makamanda wengine, yanatarajiwa kufanyika Juni 17, 2025.

Majenerali hao wamefariki ndani ya siku tatu za mashambulizi ya anga ya Israel yanayolenga maeneo mbalimbali ya Iran, ikiwa ni pamoja na viwanda vya nyuklia, viongozi wa jeshi, mitambo ya ulinzi, miji na maeneo ya mafuta.

Iran imelaani mashambulizi hayo na imeyaita tangazo la vita, huku ikijibu kwa mashambulizi ya mamia ya makombora na droni ndani ya ardhi ya Israel.

Manusura Ajali ya Ndege India: Nilidhani Nimekufa

Manusura Ajali ya Ndege India: Nilidhani Nimekufa

Raia wa Uingereza mwenye asili ya India, ndiye abiria pekee aliyepona katika ajali ya ndege ya Air India iliyokuwa ikielekea London kutoka Ahmedabad. Akiwa kitandani katika Hospitali ya Civil jijini Ahmedabad, Ramesh ameeleza kwa uchungu jinsi alivyopitia sekunde za mauti kabla ya kujiokoa.

"Ndege haikupaa vizuri, ilikuwa kama inateleza hewani tu," alisema katika mahojiano na DD News, Ijumaa. "Sekunde chache tu kabla ya kugonga jengo na kulipuka, nilihisi tunaporomoka." Ramesh, aliyekuwa kwenye kiti cha 11A kando ya dirisha, alisema upande wake wa ndege ulipata uharibifu mkubwa, na aliona ufa kwenye sehemu ya fuselage karibu na kiti chake.

"Nilidhani nimekufa. Lakini nilipoona ufa huo, nilijifungua mkanda, nikatumia mguu wangu kusukuma nikapitia hapo na kujivuta nje," alieleza.

Ajali hiyo imezusha maswali kuhusu usalama wa ndege, huku baadhi ya wataalamu wakitaka hatua kali zichukuliwe. Wataalamu wanabishana kati ya umuhimu wa ukaguzi mkali wa ndege kabla ya kuruka na mafunzo ya kina kwa marubani na hatua za dharura kama njia bora ya kuzuia ajali kama hii.

Vurugu Zasababisha Kutangazwa kwa Amri ya kutotoka Nje - Los Angeles

Vurugu Zasababisha Kutangazwa kwa Amri ya kutotoka Nje - Los Angeles

Amri ya kutotoka nje usiku imetangazwa huko Los Angeles nchini Marekani huku maafisa wa mji huo wakipambana kuyadhibiti maandamano ambayo Rais Donald Trump alidai kuwa ni uvamizi unaofanywa na adui wa kigeni.

Matukio ya uporaji na uharibifu yamekikumba kitovu cha jiji hilo la pili kwa ukubwa nchini Marekani huku maandamano ambayo kwa kiasi kikubwa yalikuwa ya amani kuhusu kukamatwa kwa wahamiaji yakigeuka kuwa vurugu nyakati za usiku ambapo Meya Karen Bass amewaambia waandishi habari kuwa amechukua hatua hiyo ili kuzuia uharibifu na uporaji.

Mitaa ya katikati ya mji wa Los Angeles itafungwa kuanzia saa mbili usiku hadi saa kumi na mbili asubuhi  huku jeshi la Polisi likimesema zaidi ya watu 500 wamekamatwa tangu maandamano yalipoanza mwishoni mwa wiki.

Maandamano pia yameshuhudiwa katika miji mingine ya Marekani ikiwemo New York, Atlanta, Chicago na San Francisco.

Trump ameamuru askari 4,000 wa Ulinzi wa Taifa kwenda Los Angeles, pamoja na wanajeshi 700 wa kitengo maalum, katika kile amedai ni hatua ya lazima ya kuchukua udhibiti  licha ya polisi wa eneo hilo kusisitiza kwamba wanaweza kushughulikia hali hiyo.

Maandamano Yazidi Kushika Kasi  Los Angeles

Maandamano Yazidi Kushika Kasi Los Angeles

Katika hali ya kusitaajabisha maandamano yamezidi kupamba moto kwa siku ya tatu huko Los Angeles  nchini Marekani ambako waandamanaji wanaopinga sera za uhamiaji za Rais wa Marekani Donald Trump wamekabiliana na maafisa wa usalama.

Wanajeshi wa kikosi maalum waliotumwa na Rais Trump mjini humo licha ya pingamizi kutoka kwa Gavana wa jimbo la California na Meya wa mji wa Los Angeles, wametumia gesi ya kutoa machozi na risasi za mpira kukabiliana na waandamanaji hao.

Meya wa Los Angeles Karen Bass amesema machafuko katika jiji hilo yaliyochochewa na utawala huku Gavana wa California Gavin Newsom akisema kuwa uamuzi wa Donald Trump kupeleka Walinzi wa Kitaifa kwenye maandamano hayo ndio uliozidisha ghasia hizo.

Waandamanaji walikusanyika karibu na eneo ambapo maafisa wa uhamiaji na utekelezaji wa Forodha walifanya uvamizi siku ya Juni 7, 2025  na kufunga barabara kuu .

 

 

Waziri wa Zamani wa Fedha wa Ghana Awekwa Kwenye Orodha ya Uhalifu

Waziri wa Zamani wa Fedha wa Ghana Awekwa Kwenye Orodha ya Uhalifu

Waziri wa zamani wa fedha wa Ghana Ken Ofori-Atta amewekwa kwenye orodha ya uhalifu ya Interpol kwa madai ya kutumia ofisi ya umma kujinufaisha binafsi.

Haya yamejiri baada ya waendesha mashtaka wa Ghana kutangaza kuwa  waziri huyo anasakwa kwa  sheria, kwa madai ya kuhusika katika kesi kadhaa za ufisadi alipokuwa serikalini.

Notisi hii sio hati ya kukamatwa bali ni ombi kwa polisi ulimwenguni kote kumzuia mtu anayesubiri kurejeshwa. Ofori-Atta anayedaiwa kuwa nje ya nchi kwa sababu za kimatibabu, hajazungumzia tuhuma hizo, lakini amesema ametendewa kinyume cha sheria.

Mzee huyo mwenye umri wa miaka 65 ameshutumiwa kwa kusababisha hasara ya kifedha kwa serikali.

Madai hayo yanajumuisha maswali kuhusu taratibu za ununuzi katika jengo la kanisa kuu la kitaifa lenye utata, ambalo limesalia kuwa shimo licha ya madai ya matumizi ya $58m (£46.6m) ya pesa za Serikali.

Mawakili wa Ofori-Atta walikuwa wamejitolea kumwakilisha lakini mwendesha mashtaka wa serikali alisema hawakuweza kujibu mashtaka ya jinai kwa niaba ya mteja wao.

Visitor Counter

000969
Today: 14
Yesterday: 3
This Week: 17
Last Week: 49
This Month: 121

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz