Msajili wa Hazina, Nehemia Mchechu amesema gawio la Serikali la mwaka 2025 ni last kihistoria ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa mwanzo yamekuja 2024, akisisitiza kuongezeka kwa gawio kutoka kwa mashirika na taasisi za umma pamoja na wabia biashara kutoka sekta binafsi.
Mchechu amesema hayo leo Juni 10, 2025, Ikulu, Dar es Salaam, wakati wa hafla ya kupokea gawio na michango kutoka kwa mashirika na taasisi za umma.
Amesema hadi kufikia Juni 9, 2025, Ofisi ya Msajili wa Hazina imekusanya shilingi trilioni 1.28 ambazo ni ongezeko la asilimia 68 ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2024 na bado makusanyo yanaendelea.
Aidha, Mchechu amesema mafanikio hayo makubwa yamewezekana kwa juhudi, usimamizi na uongozi imara wa wakurugenzi wa taasisi 213 za umma ambao wameonyesha uwajibikaji wa hali ya juu.
Mchechu ameongezea kuwa hatua hiyo ni uthibitisho kwamba taasisi za umma zinaweza kuongoza kwa uwajibikaji, ubunifu na matokeo makubwa kwa maendeleo ya Taifa.
