Mbunge wa Jimbo la Bukoba Vijijini ametoa msaada wa vifaa vya ujenzi wa jiko la wafungwa kwenye Gereza la Kilimo Rwamurumba vyenye thamani ya Sh milioni 1.3
Akizungumza wakati akikabidhi msaada huo leo Juni 17, 2025, Rweikiza amebainisha kuwa ameguswa na hadha wanayopata wafungwa wakati wa kuandaa chakula chao kwanye jiko lililoharibika hasa nyakati za mvua .
Amesema kuwa taarifa ya ubovu wa jiko hilo aliipokea kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ambaye ni Mkuu wa Wilaya, Erasto Sima ndipo akachukua uamuzi wa kuwajibika kama kiongozi.
Alitoa wito kwa jamii kujitoa kwani gereza ni sehemu inayotoa huduma za jamii kama kurekebisha makosa na kuendelea kurekebisha maadili hivyo wadau wa maendeleo wasijitenge na maeneo kama hayo.
