Iran Yatangaza Vifo vya Majenerali Sita, Yumo Mkuu wa kikosi cha Walinzi wa Mapinduzi

Iran Yatangaza Vifo vya Majenerali Sita, Yumo Mkuu wa kikosi cha Walinzi wa Mapinduzi

Kikosi Maalum cha Walinzi wa Mapinduzi nchini Iran, kimetangaza vifo vya majenerali sita hali iliyoongeza idadi ya maafisa wakuu waliouawa katika kampeni ya kijeshi ya Israel kufikia  watu wapatao16.

kwa mujibu wa shirika la habari la Tasnim lenye ushirikiano wa karibu na kikosi hicho cha Walinzi wa Mapinduzi, mazishi ya Salami, Bagheri na makamanda wengine, yanatarajiwa kufanyika Juni 17, 2025.

Majenerali hao wamefariki ndani ya siku tatu za mashambulizi ya anga ya Israel yanayolenga maeneo mbalimbali ya Iran, ikiwa ni pamoja na viwanda vya nyuklia, viongozi wa jeshi, mitambo ya ulinzi, miji na maeneo ya mafuta.

Iran imelaani mashambulizi hayo na imeyaita tangazo la vita, huku ikijibu kwa mashambulizi ya mamia ya makombora na droni ndani ya ardhi ya Israel.

Related Articles

Visitor Counter

000968
Today: 13
Yesterday: 3
This Week: 16
Last Week: 49
This Month: 120

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz