Jaji wa Umoja wa Mataifa aliyejulikana kwa jina la Lydia Mugambe (50), amehukumiwa kifungo cha miaka sita na miezi nane jela kwa kumlazimisha mwanamke kufanya kazi kama mtumwa wa nyumbani.
Lydia Mugambe alikuwa akisomea Shahada ya Uzamivu katika Chuo Kikuu cha Oxford wakati polisi walipogundua kuwa alikuwa na msichana mdogo wa Kiganda nyumbani kwake akifanya kazi isiyolipwa kama mjakazi.
Mugambe, ambaye pia ni jaji wa Mahakama Kuu nchini Uganda, alihukumiwa kufungwa katika Mahakama ya Oxford Mei 02, 2025 baada ya kupatikana na hatia ya makosa ya utumwa wa kisasa mwezi Machi.