Kiwanda cha Kuchakata Pamba Bariadi Kuongeza Ajira

Kiwanda cha Kuchakata Pamba Bariadi Kuongeza Ajira

Rais Samia Suluhu Hassan amesema hivi sasa kiwanda cha kuchakata pamba kinajengwa ambapo kitatumika kuichakata pamba ili kutengeneza nyuzi zitokanazo na pamba.

Amesema hatua hiyo itasaidia kuongeza ajira lakini pia pamba inayozalishwa ndani ya nchi kutumika hapa hapa nchini kuzalisha bidhaa nyingine badala ya kuisafirisha nje ya nchi kama ambavyo inavyofanyika sasa.

Rais Samia ameyasema hayo leo Juni 16, 2025 baada ya kuzindua kiwanda cha kuchambua pamba pamoja na kiwanda cha kutengeneza mabomba wilayani Bariadi mkoani Simiyu, ikiwa ni sehemu ya ziara yake mkoani humo.

“Tunajua kwamba Simiyu zao kubwa la kiuchumi ni pamba ukiacha mengine na nimshukuru mwekezaji hapa wa ndani amewaza kuongeza thamani angalau kwa hatua ya kwanza, lakini hatua ya pili sasa tutanunua kwake kuweka kwenye kiwanda ambacho tayari tumeanza kukijenga cha kutengeneza nyuzi za pamba. Tunataka kusitisha kupeleka pamba yetu kama ilivyo kwenye marobota kwa wenzetu wakatengeneze nguo na watu wao wapate kazi, tunataka pamba yetu tuitengeneze hapa hapa ili watu wetu wa Simiyu waweze kupata ajira ndani ya mkoa huu,” amesema Rais Samia

Related Articles

Visitor Counter

000955
Today: 3
Yesterday: 10
This Week: 3
Last Week: 49
This Month: 107

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz