Malawi yazuia  Kuingia Kwa Mazao ya Kilimo Kutoka Tanzania Waziri  Bashe atoa msimamo wake

Malawi yazuia Kuingia Kwa Mazao ya Kilimo Kutoka Tanzania Waziri Bashe atoa msimamo wake

Serikali ya Tanzania imesema imepokea taarifa rasmi kuwa Serikali ya Malawi imezuia kuingia kwa mazao ya kilimo kutoka Tanzania, yakiwemo unga, mchele, tangawizi, ndizi, na mahindi, hatua ambayo imeathiri moja kwa moja shughuli za Wafanyabiashara wa Tanzania wanaosafirisha bidhaa hizo kwenda Malawi.

Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema hayo leo April 17,2025 kupitia ukurasa wake wa X ambapo amenukuliwa akiandika “Ni vyema ifahamike kuwa kwa kipindi cha miaka mitano, Serikali ya Tanzania imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali kufungua soko la ndizi nchini Afrika Kusini bila mafanikio, hali hii inafanana na changamoto tulizopitia kwa zaidi ya miaka kumi katika kufungua soko la parachichi, hadi pale tulipoamua kuchukua hatua za kulinda maslahi ya nchi yetu”

“Kutokana na hali hii, na baada ya juhudi zote za kidiplomasia kufanyika bila mafanikio, ninapenda kuwataarifu yafuatayo, iwapo Serikali ya Malawi na Afrika Kusini hazitabadilisha msimamo wao kufikia Jumatano ijayo, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Kilimo itazuia uingizwaji wa mazao na bidhaa zote za kilimo kutoka nchi hizo mbili”

“Mizigo ya bidhaa za kilimo kutoka Malawi na Afrika Kusini haitaruhusiwa kupita ndani ya mipaka ya Tanzania, kuelekea bandari ya Dar es Salaam au nchi nyingine yoyote, hadi zuio hilo litakapoondolewa, usafirishaji wa mbolea kwenda Malawi utasitishwa, ikiwa ni sehemu ya hatua za kulinda maslahi ya wakulima na Wafanyabiashara wa Kitanzania”

“Wasafirishaji wote wa Kitanzania wanaosafirisha bidhaa za kilimo, ninawashauri kuacha kupakia bidhaa hizo mpaka hapo Malawi na Afrika Kusini watakapo badilisha msimamo wao, Wafanyabiashara walioweka order za apples, machungwa, na bidhaa zingine ambazo hununuliwa Afrika kusini, ninawashauri kuacha kwa sasa kwani hatutoziruhusu kuingia Tanzania mpaka hapo Afrika Kusini itakapo tufungulia soko la ndizi”

“Ninathibitisha kuwa kama Waziri mwenye dhamana, nimewasiliana kwa njia mbalimbali na Waziri wa Kilimo wa Malawi bila mafanikio ya kupata majibu rasmi, hatUa hizi ni za kulinda heshima ya nchi yetu, uchumi wa wakulima wetu, na usawa katika biashara za kikanda”

Related Articles

Visitor Counter

000549
Today: 5
Yesterday: 5
This Week: 5
Last Week: 54
This Month: 32

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz