Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika amesema amewasiliana na Mwenyekiti Mstaafu wa Chama hicho Freeman Mbowe na ameeleza kuwa hana dhamira ya kugombea Urais, Ubunge au uongozi wa Chama chochote cha siasa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Mnyika amesema “Natambua kuwa wachache waliojiondoa CHADEMA baadhi yao wamekuwa wakitumia jina lake kushawishi baadhi ya Viongozi wa Chama na wenye nia ya kugombea kujiondoa kwenye Chama kwa madai kuwa anawaunga mkono na anajiandaa kugombea Urais kupitia Chama kingine”
“Natambua pia mfumo wa Serikali na CCM uko nyuma ya baadhi yao kwa nia za kukwamisha no reforms no election, kupasua CHADEMA na kuhalalisha udhalimu na uharamu unaondaliwa kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025”
“Natambua kuwa mfumo huohuo ukihusisha Mtu wa karibu na Rais Samia Suluhu na Mtumishi mmoja wa Ofisi ya Msajili wa Vyama Vya Siasa ndio uliohusika kufungua kesi ya Said Issa Mohamed aliyekuwa Makamu Mwenyekiti Zanzibar na wenzake ambayo wameomba pamoja na mambo mengine shughuli za kisiasa za Chadema zizuiwe wakati kesi ya msingi ikiendelea”
“Kwa uzoefu wangu wa kuwa kwenye Sekretariati ya Chama kwa takribani miaka 21 mapito mengi ya CHADEMA ambayo tulifanikiwa kuyashinda, hii vita dhidi ya CHADEMA naamini pia tutaishinda, tuelekeze nguvu kwenye mapambano ya no reforms no election , tumjue vizuri adui yetu, tuwajue vizuri Washirika wetu, tuepuke kushambuliana sisi kwa sisi mpaka iwepo sababu ya kweli na ya lazima yakufanya hivyo, kwa umoja na nguvu ya pamoja, tutashinda”
