Rais Samia Achangia Milioni 50 Ujenzi wa Kanisa Katoliki Kigoma

Rais Samia Achangia Milioni 50 Ujenzi wa Kanisa Katoliki Kigoma

RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa kiasi cha Sh milioni 50 kuchangia ujenzi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Maria Mtakatifu Mwana wa Mungu Kibwigwa Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma ambapo kiasi cha Sh milioni 250.2 kilichangwa katika harambee hiyo.

Akitangaza matokeo ya harambee hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli (TRC), Masanja Kadogosa ambaye mgeni rasmi alichangia Sh milioni 20. Amesema Rais Samia kwa mapenzi mema amechangia ujenzi huo baada ya kuombwa kufanya hivyo na askofu wa jimbo la Kigoma Mhashamu Askofu Mlola.

Kadogosa amesema kuwa katika harambee hiyo Rais Samia pia aliungwa mkono na Mwenyekiti wa kampuni ya GSM, Gharib Mohamed huku wapenzi wa timu za Simba na Yanga waumini wa kanisa hilo wakichangia kiasi cha Sh 890,000 ambapo wapenzi wa Yanga walichangia Sh 528,000 na wapenzi wa Simba Sh 362,000.

Awali Askofu wa jimbo Katoliki la Kigoma, Mhashamu Joseph Mlola alimshukuru Rais Samia kwa mchango huo na kuongeza kuwa ni kiongozi anayejali watu kwa hali yeyote sambamba na kuwashukuru wote waliofaanikisha harambee hiyo wakiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa.

Related Articles

Visitor Counter

000727
Today: 8
Yesterday: 4
This Week: 8
Last Week: 91
This Month: 210

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz