REA Wakoshwa Nishati Safi ya Kupikia Gereza la Maweni

REA Wakoshwa Nishati Safi ya Kupikia Gereza la Maweni

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imeridhishwa na juhudi zilizochukuliwa na Magereza Mkoa wa Tanga kwa kuanza kutumia Nishati Safi ya Kupikia katika kuandaa chakula cha wafungwa wa zaidi ya 560 tofauti na hapo awali ambapo matumizi ya kuni na mkaa yalikuwa ni zaidi ya asilimia 100.

Akizungumza baada ya kutembelea Gereza la Maweni mkoani Tanga leo Mei 13, Balozi Radhia Msuya, amesema Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imeridhishwa kwa kiwango kikubwa na hatua zilizochukuliwa Magereza mkoani humo katika kutekeleza agizo lililotolewa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, mwaka mmoja uliopita kuwa taasisi zote zinazowahudumia watu zaidi ya 100 kuacha kutumia nishati chafu (kuni na mkaa) ili kupunguza matumizi ya kuni na mkaa ambayo yanachangia uharibifu wa mazingira.

Baada ya kutembelea na kujionea miundombinu ya Nishati Safi ya Kupikia katika gereza hilo, Wajumbe wa Bodi REB, Wakili Mwantum Sultan na James Mabula, wamesema wameridhishwa kwa hatua zilizochukuliwa na taasisi hiyo na kuongeza kuwa juhudi hizo, zitasaidia kufikia lengo la agizo la Rais Samia ambapo Magereza Tanzania Bara yatapata Sh bilioni 35 kama ruzuku kutoka serikalini kupitia REA ili kutekelezaji wa miradi mbalimbali ya Nishati Safi ya Kupikia.

Kwa upande wake, Mkuu wa Magereza Tanga, ACP, Fredrick Massawe amesema magereza imejiwekea malengo endelevu ya matumizi ya Nishati Safi huku akishukuru ushirikiano uliopo baina yao na REA ambao utawezesha Magereza kupata majiko banifu, mitungi ya gesi ya LPG, upatikanikanaji wa mkaa banifu (Rafiki Briquettes) pamoja na ununuzi wa mashine 61 za kutengeneza mkaa mbadala pamoja na kukuza uwezo kwa Watumishi 280 wa Magereza kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Naye Meneja Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi ya Nishati Safi, Mhandisi, Emmanuel Yesaya kutoka REA amesema, tarehe 13 Septemba mwaka jana REA ilisaini mkataba na Magereza ambapo Serikali itatoa ruzuku kwa ajili ya kuwezesha uboreshaji wa miundombinu ya Nishati Safi ya kupikia kwa Magereza yote Tanzania Bara ambapo utekelezaji ukaanza mwezi Desemba, 2025 na uda wa utekelezaji wa mradi huo utakuwa miezi 36 huku gharama ya mradi itakuwa Sh bilioni 35.

Related Articles

Visitor Counter

000727
Today: 8
Yesterday: 4
This Week: 8
Last Week: 91
This Month: 210

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz