Samamba Ataka Ubunifu Zaidi Sekta ya Madini

Samamba Ataka Ubunifu Zaidi Sekta ya Madini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba amewataka watendaji wa Tume ya Madini kuongeza ubunifu kwenye usimamizi wa Sekta ya Madini hasa katika kuongeza ushiriki wa watanzania katika Sekta ya Madini kupitia shughuli za utafiti, uchimbaji, uchenjuaji na biashara ya madini sambamba na utoaji wa huduma kwenye shughuli za uchimbaji wa madini.

Mhandisi Samamba ametoa kauli hiyo leo Mei 13, 2025 kwenye ufunguzi wa mafunzo kwa makamishna wapya wa Tume ya Madini jijini Dodoma yenye lengo la kuwajengea uelewa kuhusu Sekta ya Madini sambamba na majukumu ya Tume ya Madini.

Makamishna wapya walioteuliwa hivi karibuni na Rais Samia Suluhu Hassan ni Mhandisi Theonestina Mwasha na Dk. Theresia Numbi.

Samamba amesema kuwa tangu kuanzishwa kwa Tume ya Madini Aprili 2018 ushiriki wa watanzania katika Sekta ya Madini umeongezeka na kupungua kwa migogoro kwenye shughuli za uchimbaji wa madini na kuwataka Makamishna wapya kuendelea kubuni mikakati mipya ya kuhakikisha watanzania wengi wanashiriki kwenye shughuli za madini ikiwa ni pamoja na utoaji wa huduma kwenye migodi ya madini.

“Pamoja na mafanikio makubwa yaliyopatikana hususan ushiriki mkubwa wa watanzania kwenye Sekta ya Madini na kupungua kwa migogoro kwenye shughuli za uchimbaji wa madini, ninawataka kuongeza ubunifu hasa kwenye usimamizi wa eneo la utoaji wa leseni za madini, ushiriki wa watanzania katika Sekta ya Madini na wajibu wa Kampuni za Madini kwa Jamii (CSR) ili mchango wa Sekta ya Madini kwenye Pato la Taifa uendelee kukua.” Amesema.

Akielezea mafanikio katika Sekta ya Madini kwa kifupi, Mhandisi Samamba amesema kuwa tangu kuanzishwa kwa Tume ya Madini mafanikio makubwa yamepatikana ikiwa ni pamoja na uanzishwaji wa Ofisi za Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa 30, Maafisa Migodi Wakazi 13, Masoko ya Madini 43 na Vituo vya Ununuzi wa Madini 109.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Dk. Janet Lekashingo amewapongeza makamishna wapya kwa uteuzi uliofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan na kuahidi ushirikiano kutoka kwa watendaji na watumishi wa Tume ya Madini.

Related Articles

Visitor Counter

000727
Today: 8
Yesterday: 4
This Week: 8
Last Week: 91
This Month: 210

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz