Tume Yaundwa Kujadili Kinga ya Aliyekuwa Rais Joseph Kabila

Tume Yaundwa Kujadili Kinga ya Aliyekuwa Rais Joseph Kabila

Tume Maalum umeundwa katika bunge la Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo, kuanza kujadili suala la kuondolewa kwa kinga ya kutokamatwa kwa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Joseph Kabila.

Tume hiyo ina masaa 72 kuwasilisha ripoti yake kwa bunge la Seneta.

Mjadala huo uliofanyika wakati wa kipindi cha kikao maalum jana, Alhamisi.

Hata hivyo, inadaiwa kuwa na mgawanyiko bungeni wengine wakiunga mkono hoja hiyo ilihali wengine wakirejelea kifungu cha 224 cha sheria za utaratibu wa Seneti, wakiamini kwamba utaratibu huu unapaswa kuwasilishwa kwa kupigiwa kura bungeni.

Ikiwa hoja ya kutaka aondolewe kinga itaungwa mkono, atapoteza hadhi yake ya kuwa seneta wa kudumu na hivyo basi kuweza kushtakiwa.

Kabila anashukiwa kuwa na uhusiano na Congo River Alliance, muungano wa makundi ya waasi.

Anashtakiwa kwa uhaini, uhalifu wa kivita, uhalifu dhidi ya binadamu, na kushiriki katika harakati za uchochezi.

Vitendo hivyo vinadaiwa kutokea baada ya muda wake wa urais.

Related Articles

Visitor Counter

000970
Today: 1
Yesterday: 14
This Week: 18
Last Week: 49
This Month: 122

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz