Vurugu Zasababisha Kutangazwa kwa Amri ya kutotoka Nje - Los Angeles

Vurugu Zasababisha Kutangazwa kwa Amri ya kutotoka Nje - Los Angeles

Amri ya kutotoka nje usiku imetangazwa huko Los Angeles nchini Marekani huku maafisa wa mji huo wakipambana kuyadhibiti maandamano ambayo Rais Donald Trump alidai kuwa ni uvamizi unaofanywa na adui wa kigeni.

Matukio ya uporaji na uharibifu yamekikumba kitovu cha jiji hilo la pili kwa ukubwa nchini Marekani huku maandamano ambayo kwa kiasi kikubwa yalikuwa ya amani kuhusu kukamatwa kwa wahamiaji yakigeuka kuwa vurugu nyakati za usiku ambapo Meya Karen Bass amewaambia waandishi habari kuwa amechukua hatua hiyo ili kuzuia uharibifu na uporaji.

Mitaa ya katikati ya mji wa Los Angeles itafungwa kuanzia saa mbili usiku hadi saa kumi na mbili asubuhi  huku jeshi la Polisi likimesema zaidi ya watu 500 wamekamatwa tangu maandamano yalipoanza mwishoni mwa wiki.

Maandamano pia yameshuhudiwa katika miji mingine ya Marekani ikiwemo New York, Atlanta, Chicago na San Francisco.

Trump ameamuru askari 4,000 wa Ulinzi wa Taifa kwenda Los Angeles, pamoja na wanajeshi 700 wa kitengo maalum, katika kile amedai ni hatua ya lazima ya kuchukua udhibiti  licha ya polisi wa eneo hilo kusisitiza kwamba wanaweza kushughulikia hali hiyo.

Related Articles

Visitor Counter

000969
Today: 14
Yesterday: 3
This Week: 17
Last Week: 49
This Month: 121

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz