Waziri wa Afya Ashitua Jambo Hospitali ya Rufaa

Waziri wa Afya Ashitua Jambo Hospitali ya Rufaa

Waziri wa Afya, Jenista Mhagama amemuagiza Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk Seif Shekalage kutuma timu ya wataalamu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kwenda katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu kufanya ukaguzi na kuangalia kama mfumo wa Tehama unafanya kazi ipasavyo.

Jenista alitoa maagizo hayo jana baada ya kufanya ziara ya kutembelea na kukagua miundombinu katika hospitali hiyo kisha kuzungumza na watumishi.

Alisema mfumo wa Tehama kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ni muhimu katika kuongeza ufanisi wa utoaji huduma bora za afya kwa wananchi, ikiwemo kuweka ulinzi na usalama wa miundombinu ya hospitali.

Alisema alipewa taarifa na uongozi wa hospitali hiyo kuwa wamekuwa wakitumia walinzi kufuatilia upotevu wa baadhi ya vitu, utaratibu ambao alisema umepitwa na wakati kwani kila kitu kinaendeshwa kwa Tehama.

“Hospitali hii imewekwa mifumo ya Tehama, kama mfumo wetu umeunganishwa idara zote za hospitali inakuwaje tushindwe kudhibiti mwenendo mzima wa shughuli zote zinazofanyika kwenye hospitali yetu?” Alihoji.

Related Articles

Visitor Counter

000955
Today: 3
Yesterday: 10
This Week: 3
Last Week: 49
This Month: 107

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz