"Wiki ya afya inaweka Mikakati ya pamoja ya kuboresha huduma za afya nchini" Dkt. Dugange

"Wiki ya afya inaweka Mikakati ya pamoja ya kuboresha huduma za afya nchini" Dkt. Dugange

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Dkt. Festo Dugange, amesema wiki ya afya ni muhimu kwa kuwa inatoa fursa ya kujikumbusha na kuweka mikakati ya pamoja ya kuboresha huduma za afya nchini.

Akizungumza katika kilele cha wiki hiyo jijini Dodoma Aprili 8, 2025 kwa niaba ya Waziri wa TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amesema Serikali imeendelea kufanya maboresho makubwa katika sekta ya afya kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na za uhakika, huku akimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa maono yake makubwa katika kuiinua sekta hiyo.

“Huduma za afya zinaendelea kuimarika kupitia uwekezaji kwenye vifaa tiba na miundombinu. Katika kipindi cha miaka minne iliyopita, zaidi ya shilingi trilioni moja zimetumika kuboresha huduma za afya katika ngazi ya msingi,” amesisitiza Dkt. Dugange.

Aidha, Naibu Waziri Dugange amewapongeza watumishi wa sekta ya afya kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya na kuhimiza kuendelea kushirikiana kwa karibu katika kuhakikisha huduma za afya zinafikia kila mtanzania kwa ubora unaotakiwa.

Related Articles

Visitor Counter

000531
Today: 5
Yesterday: 9
This Week: 41
Last Week: 32
This Month: 14

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz