Papa Francis Afariki Dunia leo Aprili 21, 2025

Papa Francis Afariki Dunia leo Aprili 21, 2025

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis, amefariki Dunia leo Aprili 21,2025 kwenye Jumatatu ya Pasaka akiwa na umri wa miaka 88 ambapo Vatican imethibitisha na kusema Papa amefia kwenye makazi yake Vatican na taarifa zaidi kuhusu kifo chake zitatolewa.

Papa ambaye alizaliwa mwaka 1936 hivi karibuni amepitia changamoto ya upumuaji hadi kuhitaji mashine ya kusaidia kupumua na amekuwa akikabiliwa na matatizo ya kiafya ikiwemo maambukizi ya mapafu(nimonia) hadi kupelekea kulazwa kwa wiki kadhaa kabla ya baadaye afya yake kuimarika

Viongozi wa Marekani, EU na Ukraine kukutana mjini Paris

Viongozi wa Marekani, EU na Ukraine kukutana mjini Paris

viongozi wa ngazi za juu wa Marekani, umoja wa Ulaya na Ukraine, wanatarajia kukutana alhamisi mjini Paris nchini Ufaransa , kujadili hatma ya mzozo kati ya Urusi na Ukraine na kukwama kwa juhudi za amani.

mkutano huo utahudhuriwa na waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio, mjumbe maalum wa  Rais wa Marekani , Steve Witkoff, Rais wa Ufaransa  Emmanuel Macron na waziri wake wa mambo ya nje Jean-Noel Barrot.

Ukraine itawakilishwa na waziri wake wa mambo ya nje Andrii Sybiha pamoja na mkuu wa ofisi ya rais Andriy Yermak ambaye amesema watakutana pia kwa mazungumzo na viongozi wa Ujerumani na Uingereza kuhusu suala la dhamana ya usalama ikiwa kutafikiwa mpango wa amani.

Trump atangaza kusitisha nyongeza ya ushuru kwa siku 90

Trump atangaza kusitisha nyongeza ya ushuru kwa siku 90

Rais Donald Trump ametangaza kusitisha kwa siku 90 nyongeza ya ushuru kwa bidhaa zinazoingizwa Marekani kutoka mataifa mengine huku akikosa kuilegezea China.

Katika mabadiliko makubwa ya sera, saa chache baada ya ushuru dhidi ya takriban washirika 60 wa biashara wa Marekani kuanza, Trump alisema alikuwa akiidhinisha "kupunguzwa kwa ushuru wa asilimia 10%" wakati mazungumzo yakiendelea.

Hata hivyo aliongeza ushuru wa forodha kwa bidhaa kutoka China hadi asilimia 125%, akiishutumu Beijing kwa "ukosefu wa heshima" baada ya kulipiza kisasi kwa kusema kuwa ingetoza ushuru wa 84% kwa bidhaa za Marekani.

"Itafika wakati China igundue kuwa siku za kuvuna kutoka kwa Marekani na nchi zingine sio endelevu au kukubalika," anasema Trump.

Waziri wa Fedha wa Marekani Scott Bessent alisisitiza kuwa mabadiliko ya sera hayajaathiriwa na anguko la kimataifa la kiuchumi, lakini mwandamizi wa chama cha Democrat Chuck Schumer alisema uamuzi huo unaonyesha Trump anayumba na kurudi nyuma.

Akihojiwa na waandishi wa habari kuhusu athari za kujibizana na China kibiashara,  Trump amesema anaamini watafikia makubaliano na kiongozi wa China.

"Nadhani Rais Xi ni mtu anayefahamu fika anachokifanya.Ni mwerevu,anaipenda nchi yake,hilo nafahamu vyema,namjua vizuri na nadhani atataka kufikia makubaliano,nadhani hilo litafanyika.Tutapata simu wakati fulani na kutaafikiana,litakuwa jambo jema kwa na kwetu na litakuwa jambo jema kwa ulimwengu na ubinadamu", ameongeza Trump.

Hata hivyo, uamuzi huu mpya wa Trump haujaathiri tangazo la awali la ushuru ambao unaendelea kutekelezwa tangu tarehe 2 mwezi Aprili ikiwa ni ni pamoja na asilimia 25% ya ushuru wa kuagiza kwa magari na vipuri vya magari vinavyoingia Marekani, na ushuru zaidi wa 25% kwa bidhaa zote za chuma na alumini.

Ushuru wa kimataifa wa Trump umesababisha msukosuko mkubwa zaidi wa biashara ambao hujawahi kutokea katika miongo kadhaa.

Wastaafu na wataalam wa maendeleo  watoa  wito  kwa Serikali juhudi za uhifadhi wa mazingira

Wastaafu na wataalam wa maendeleo watoa wito kwa Serikali juhudi za uhifadhi wa mazingira


Viongozi wastaafu barani Afrika pamoja na wataalam wa maendeleo wametoa wito kwa Serikali barani humo kutekeleza mikakati inayotambua na kutoa motisha kwa watu wanaowekeza katika juhudi za uhifadhi wa mazingira.

Wito huo umetolewa Aprili 8,2025 katika Jiji la Kampala nchini Uganda katika siku ya pili ya Mkutano wa 8 wa Viongozi wa Afrika (ALF), unaoendelea chini ya uratibu wa Taasisi ya Uongozi (Uongozi Institute).

Mlezi wa Kongamano hilo na Rais wa Mstaafu wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, amesisitiza umuhimu wa mataifa ya Afrika kuwawezesha wananchi wao, hususani wataalam wa majadiliano wa masuala ya mazingira ili waweze kushiriki kikamilifu katika majukwaa ya kimataifa.

“Tunaponyimwa fursa ya kutumia ipasavyo rasilimali zetu na badala yake zikanufaisha mataifa yenye nguvu kiuchumi, tunajikuta tukikosa uwezo wa kushughulikia changamoto kama mabadiliko ya tabia nchi na uhifadhi wa misitu” 

“Tunatoa motisha kwa watu wanaopanda miti mipya lakini hatuwatambui wala kuwathamini wale wanaolinda misitu iliyopo. Hii inaleta pengo kubwa katika juhudi za uhifadhi na kudhoofisha azma ya kulinda ikolojia ya asili.” amesema Rais mstaafu Kikwete.

Amesisitiza kuwa mfumo wa sasa ambao unamnufaisha kifedha mharibifu wa mazingira huku mhifadhi akikosa chochote hauwezi kudumu. “Ni lazima  mataifa hayo yabadilishe mtazamo huu kwa kutambua mchango wa misitu katika kuhifadhi kaboni.


Kupunguzwa kwa bajeti za misaada kwawaweka hatarini wajawazito

Kupunguzwa kwa bajeti za misaada kwawaweka hatarini wajawazito

Umoja wa Mataifa umeonya kuwa kupunguzwa kwa bajeti za misaada kutahujumu hatua zilizokuwa zimefanikishwa za kupunguza vifo vya kina mama wakati wa kujifungua.

Ripoti iliyotolewa na Shirika la Afya Duniani (WHO) imesema vifo vitokanavyo na ujauzito na kujifungua vilikuwa vimeshuka kwa asilimia arobaini katika karne hii lakini wataalam wanahofu kuwa huwenda vifo hivyo vikaongezeka tena kutokana na kusitishwa kwa misaada ya kigeni.

Wanawake walio na ujauzito hukumbwa na changamoto nyingi hasa katika mataifa yanayokumbwa na mizozo kama Chad, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Nigeria na Somalia.

Mnamo mwaka 2020,WHO ilirekodi vifo zaidi ya  laki mbili  ikiwa ni sawa na mwanamke mmoja kufariki Dunia kila baada ya dakika mbili kutokana na changamoto wakati wa kujifungua.

Kifo cha uzazi ni kile kinachosababishwa na matatizo wakati wa ujauzito au ndani ya wiki sita baada ya mwisho wake huku sababu zinazoongoza katika vifo hivyo ikiwa  ni pamoja na kutokwa na damu nyingi, maambukizi kama vile malaria, matatizo wakati wa kujifungua, na utoaji mimba usio salama.

Visitor Counter

000536
Today: 5
Yesterday: 5
This Week: 46
Last Week: 32
This Month: 19

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz