, Constant Mutamba, anakabiliwa na tuhuma za matumizi mabaya ya takriban dola milioni 20 za Marekani, ambazo zilikuwa zimekusudiwa kwa ajili ya ku.jpg)
Waziri wa Sheria wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Constant Mutamba, anakabiliwa na tuhuma za matumizi mabaya ya takriban dola milioni 20 za Marekani, ambazo zilikuwa zimekusudiwa kwa ajili ya kufidia waathirika wa vita vinavyoendelea mashariki mwa nchi hiyo.
Taarifa hizo zilitolewa jana na Spika wa Bunge la DRC, Vital Kamerhe, ambaye amesema kuwa bunge limeanzisha mchakato wa kumhoji Waziri Mutamba kupitia tume maalum ya uchunguzi, ambayo itaundwa na wabunge watakaotangazwa hivi karibuni.
“Tumeunda tume maalum ya kibunge kwa ajili ya kumhoji Waziri wa Sheria kuhusu tuhuma hizi nzito zinazohusu fedha zilizotengwa kwa fidia ya waathirika wa migogoro ya kijeshi mashariki,” alisema Kamerhe.

Baraza la Seneti nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limepiga kura ya kumuondolea kinga ya kutoshitakiwa rais wa zamani Joseph Kabila anayeshutumiwa na serikali kwa kuwasaidia waasi waliopo mashariki mwa Kongo.
Kura 88 zilipigwa kuunga mkono hatua hiyo itakayopelekea kiongozi huyo wa zamani kushitakiwa kwa kuwaunga mkono M23.
Spika wa Baraza la Seneti Jean-Michel Sama Lukonde alitangaza baada ya kura hiyo kwamba sasa baraza hilo limeruhusu Kabila kushitakiwa na kuondolewa kinga.
Rais Felix Tshisekedi aliyeshika usukani baada ya Kabila, anamtuhumu mtangulizi wake huyo kwa kushirikiana na M23 waliolikamata eneo kubwa la mashariki mwa Kongo.