Ramaphosa Asifiwa kwa Busara Dhidi ya Trump

Ramaphosa Asifiwa kwa Busara Dhidi ya Trump

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amesifiwa nyumbani kwa jinsi alivyosimama kwa utulivu na staha mbele ya tuhuma nzito na zisizo na msingi alizorushiwa na Rais wa Marekani, Donald Trump.

Katika moja ya matukio yaliyozua taharuki, Trump alimwonyesha Ramaphosa video yenye madai ya "mauaji ya halaiki dhidi ya wakulima wazungu" nchini Afrika Kusini madai ambayo yamekanushwa mara kwa mara na Pretoria na ambayo wataalamu wameyaeleza kuwa ya kupotosha.

Lakini licha ya mtego huo wa kisiasa, Ramaphosa alijibu kwa utulivu, na hata kumzawadia Trump kitabu kuhusu mchezo wa gofu.

Watetezi wa haki za binadamu na raia wa kawaida walitoa kauli za kuunga mkono mtindo wa Ramaphosa.

Wengine walitaka majibu makali zaidi dhidi ya uongo huo, lakini wengi waliona uongozi wake kama kielelezo cha diplomasia ya kweli “Nadhani nchi yetu imejieleza vyema na kuweka ukweli mezani,” alisema mwanaharakati Ulrich Steenkamp.

Kwa upande wa matokeo ya kisiasa, Ramaphosa alisema mkutano wao umefungua mlango kwa mazungumzo ya kina kuhusu biashara na ushirikiano kati ya mataifa hayo mawili.

Marekani ni mshirika wa pili kwa ukubwa wa kibiashara kwa Afrika Kusini baada ya China, na hatua ya Marekani kuashiria kuanza tena majadiliano ya biashara ilipokelewa kama mafanikio makubwa kwa Ramaphosa.

Mwamba Mutamba Kuhojiwa

Mwamba Mutamba Kuhojiwa

Waziri wa Sheria wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Constant Mutamba, anakabiliwa na tuhuma za matumizi mabaya ya takriban dola milioni 20 za Marekani, ambazo zilikuwa zimekusudiwa kwa ajili ya kufidia waathirika wa vita vinavyoendelea mashariki mwa nchi hiyo.

Taarifa hizo zilitolewa jana na Spika wa Bunge la DRC, Vital Kamerhe, ambaye amesema kuwa bunge limeanzisha mchakato wa kumhoji Waziri Mutamba kupitia tume maalum ya uchunguzi, ambayo itaundwa na wabunge watakaotangazwa hivi karibuni.

“Tumeunda tume maalum ya kibunge kwa ajili ya kumhoji Waziri wa Sheria kuhusu tuhuma hizi nzito zinazohusu fedha zilizotengwa kwa fidia ya waathirika wa migogoro ya kijeshi mashariki,” alisema Kamerhe.

Uhuru wa Watu wa Afrika Mashariki Unadorora - Karua

Uhuru wa Watu wa Afrika Mashariki Unadorora - Karua

Waziri wa zamani wa Sheria nchini Kenya Martha Karua amesema anadhani uhuru wa raia katika eneo la Afrika Mashariki unadorora.

Uhuru wa Watu wa Afrika Mashariki Unadorora - Karua

Uhuru wa Watu wa Afrika Mashariki Unadorora - Karua

Waziri wa zamani wa Sheria nchini Kenya Martha Karua amesema anadhani uhuru wa raia katika eneo la Afrika Mashariki unadorora.

Kabila Aondolewa Kinga ya Kutoshitakiwa

Kabila Aondolewa Kinga ya Kutoshitakiwa

Baraza la Seneti nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limepiga kura ya kumuondolea kinga ya kutoshitakiwa rais wa zamani Joseph Kabila anayeshutumiwa na serikali kwa kuwasaidia waasi waliopo mashariki mwa Kongo.

Kura 88 zilipigwa kuunga mkono hatua hiyo itakayopelekea kiongozi huyo wa zamani kushitakiwa kwa kuwaunga mkono M23.

Spika wa Baraza la Seneti Jean-Michel Sama Lukonde alitangaza baada ya kura hiyo kwamba sasa baraza hilo limeruhusu Kabila kushitakiwa na kuondolewa kinga.

Rais Felix Tshisekedi aliyeshika usukani baada ya Kabila, anamtuhumu mtangulizi wake huyo kwa kushirikiana na M23 waliolikamata eneo kubwa la mashariki mwa Kongo.

Visitor Counter

000969
Today: 14
Yesterday: 3
This Week: 17
Last Week: 49
This Month: 121

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz