Mahakama ya Kongo Yamhukumu Matata Ponyo Miaka 10 Jela

Mahakama ya Kongo Yamhukumu Matata Ponyo Miaka 10 Jela

Waziri mkuu wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Augustin Matata Ponyo amehukumiwa kifungo cha miaka kumi jela na kazi ngumu baada ya kutiwa hatiani kwa ufisadi.

Kufuatia mapambano ya kisheria yaliyodumu karibu miaka minne, mahakama ya katiba ya Kongo ilimkuta Matata ana hatia kwa ubadhirifu wa fedha za umma za thamani ya dola milioni 247.

Matata, ambaye alifanya kampeni dhidi ya rais wa sasa wa Kongo Felix Tshisekedi mwaka 2023 kabla kujiondoa katika kinyang'anyiro cha urais, amekuwa mara kwa mara akikanusha madai hayo akiyaeleza kuwa yamechochewa kisiasa.

Kando na Matata, jaji aliyesikiliza kesi hiyo Dieudonne Kamuleta alimhukumu mfanyabiashara wa Afrika Kusini kifungo cha miaka mitano jela na kazi ngumu na Deogratias Mutombo, ambaye wakati huo alikuwa gavana wa benki kuu ya Kongo.

Matata na Mutombo wamepigwa marufuku wasishike nyadhifa katika ofisi za umma kwa miaka mitano baada ya kukamilisha adhabu yao ya kazi ngumu.

Mfanyabiashara wa Afrika Kusini ameamriwa arudishwe kwao baada ya kutumikia kifungo chake.

Tume Yaundwa Kujadili Kinga ya Aliyekuwa Rais Joseph Kabila

Tume Yaundwa Kujadili Kinga ya Aliyekuwa Rais Joseph Kabila

Tume Maalum umeundwa katika bunge la Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo, kuanza kujadili suala la kuondolewa kwa kinga ya kutokamatwa kwa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Joseph Kabila.

Tume hiyo ina masaa 72 kuwasilisha ripoti yake kwa bunge la Seneta.

Mjadala huo uliofanyika wakati wa kipindi cha kikao maalum jana, Alhamisi.

Hata hivyo, inadaiwa kuwa na mgawanyiko bungeni wengine wakiunga mkono hoja hiyo ilihali wengine wakirejelea kifungu cha 224 cha sheria za utaratibu wa Seneti, wakiamini kwamba utaratibu huu unapaswa kuwasilishwa kwa kupigiwa kura bungeni.

Ikiwa hoja ya kutaka aondolewe kinga itaungwa mkono, atapoteza hadhi yake ya kuwa seneta wa kudumu na hivyo basi kuweza kushtakiwa.

Kabila anashukiwa kuwa na uhusiano na Congo River Alliance, muungano wa makundi ya waasi.

Anashtakiwa kwa uhaini, uhalifu wa kivita, uhalifu dhidi ya binadamu, na kushiriki katika harakati za uchochezi.

Vitendo hivyo vinadaiwa kutokea baada ya muda wake wa urais.

Bunge la Uganda Laidhinisha Matumizi ya Serikali ya 2025/26 Yaliyopendekezwa

Bunge la Uganda Laidhinisha Matumizi ya Serikali ya 2025/26 Yaliyopendekezwa

Wabunge wa Uganda wameidhinisha bajeti inayopendekezwa na serikali kwa mwaka wa fedha unaoanza Julai.

Nchi hiyo ya Afrika Mashariki itatumia shilingi trilioni 72.4 za Uganda (dola bilioni 20) katika mwaka wa fedha wa 2025/26 (Julai-Juni), ikiwa ni mabadiliko kidogo kutoka kwa matumizi ya mwaka unaoishia mwezi ujao ambayo yanafikia shilingi trilioni 72.1, bunge lilisema kwenye ujumbe wa mtandao wa kijamii wa X Mei 15, 2025.

"Bunge limezingatia na kupitisha mapendekezo ya bajeti ya mwaka ya fedha 2025/2026," ilisema.

Bunge halikusema ni sekta zipi zitapokea fedha nyingi lakini serikali iliwahi kusema siku za nyuma, vipaumbele vya matumizi katika mwaka ujao wa fedha vitakuwa katika sekta ya kilimo, utalii na madini yakiwemo mafuta ya petroli.

Waziri wa Fedha Matia Kasaija anatazamiwa kuwasilisha bajeti hiyo bungeni rasmi Juni 12 na kutoa maelezo zaidi kuhusu mahali pesa hizo zitatumika.

Uganda inatekeleza miradi ya miundombinu ili kuanza uzalishaji wa kibiashara wa mafuta ghafi mwaka ujao.

Miundombinu hiyo inajumuisha bomba la mafuta ghafi lenye thamani ya dola bilioni 5 kusaidia nchi hiyo isiyo na bandari kusafirisha mafuta yake kwenye masoko ya kimataifa kupitia Tanzania.

Sudan Kusini Yakanusha Ripoti za Kifo cha Rais Salva Kiir

Sudan Kusini Yakanusha Ripoti za Kifo cha Rais Salva Kiir

Baada ya kusambaa kwa uvumi mitandaoni juu ya taarifa za kifo cha  Rais Salva Kiir, Serikali ya Sudan Kusini imekanusha imekanusha uvumi huo na kusema kuwa sio kweli.

 
 
 Cyril Ramaphosa Kukutana na Rais wa Marekani Wiki Ijayo

Cyril Ramaphosa Kukutana na Rais wa Marekani Wiki Ijayo

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa  anatarajia kukutana na Rais wa Marekani Donald Trump wiki ijayo nchini Marekani katika  ziara rasmi.

Trump amekata misaada yote ya kifedha ya Marekani kwa Afrika Kusini, akikosoa sera yake ya mageuzi ya umiliki wa ardhi na kesi ya mauaji ya halaiki ambayo Afrika Kusini iliiwasilisha katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu ICC dhidi ya Israel, nchi ambayo ni mwandani wa Marekani.

Wiki hii utawala wa Trump uliwakaribisha Marekani, Waafrika Kusini 49 weupe, ukisema wamekuwa wahanga wa ubaguzi wa rangi huko Afrika Kusini huku Serikali ya Afrika Kusini ikikanusha madai ya Trump ikisema hakuna ushahidi wa kuteswa kwa Waafrika Kusini weupe nchini humo.

Visitor Counter

000969
Today: 14
Yesterday: 3
This Week: 17
Last Week: 49
This Month: 121

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz