Marekani Yapunguza Msaada kwa Zambia Kutokana na Wizi wa Dawa na Vifaa Tiba

Marekani Yapunguza Msaada kwa Zambia Kutokana na Wizi wa Dawa na Vifaa Tiba

Marekani imetangaza  kupunguza msaada wa $50m (£37m) kwa sekta ya afya ya Zambia, kutokana na nchi hiyo kushindwa kushughulikia wizi wa kimfumo wa dawa na vifaa tiba vilivyotolewa.

Uamuzi huu mgumu ulichukuliwa baada ya onyo la mara kwa mara kwa Serikali ya Zambia kulinda dawa muhimu kwa ajili ya wagonjwa walio hatarini zaidi nchini humo,

Hatua hii ya Marekani kwa Zambia ni tofauti na kusitishwa kwa misaada ya kigeni iliyotangazwa na Rais Donald Trump mnamo Januari.

 

Zaidi ya maduka ya dawa 2,000 kote nchini Zambia yalipatikana yakiuza dawa na vifaa tiba vilivyotolewa katika uchunguzi wa mwaka mzima uliofanywa na ubalozi wa Marekani.

Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya taarifa  vimeeleza kuwa kwa hali ya kushangaza,  asilimia 95 ya maduka ya dawa yaliyokuwa yakiuza aina ya bidhaa ambazo Marekani hutoa, pia walikuwa wakiuza bidhaa za wizi.

Takribani nusu ya maduka ya dawa yaliyotembelewa yalipatikana yakiuza dawa na vifaa vilivyotolewa na serikali ya Marekani hukun maduka mengine ya dawa pia yalikuwa yakiuza hisa za matibabu zilizoibiwa  na kununuliwa na serikali ya Zambia, Mfuko wa dunia na wafadhili wengine.

Waafrika Watatu Wanaotajwa Katika Uchaguzi wa Papa

Waafrika Watatu Wanaotajwa Katika Uchaguzi wa Papa

Kongamano ambalo limepigiwa kura na Makadinali wa Kanisa Katoliki kumchagua Papa mpya, limeanza vikao mnamo Mei 7 2025 huku vikao vya faragha vikifanyika katika Kanisa la Sistine na kuhudhuriwa na  Makadinali  wapatao 135.

Haijulikani itachukua muda gani kumchagua Papa, lakini mikutano miwili ya awali iliyofanyika mwaka 2005 na 2013, ilidumu kwa siku mbili pekee.

 

Wakiwa ndani ya kanisa la Sistine, Makadinali hawatakiwi kuwasiliana na ulimwengu wa nje hadi Papa mpya atakapochaguliwa.

Kuna duru moja tu ya upigaji kura siku ya kwanza katika majira ya alasiri. Kuanzia siku ya pili na kuendelea, Makadinali hupiga kura mara mbili kila asubuhi na mara mbili kila alasiri katika kanisa.

Ili kuchaguliwa kuwa Papa, mgombea lazima apate thuluthi mbili ya kura za wapiga kura Makardinali.

Wakati wa kupiga kura, kila mpiga kura huandika jina la mgombea anayempendelea kwenye karatasi ya kura chini ya maneno "Ninamchagua kama Papa Mkuu."

Ili kuhifadhi usiri wa kura, Makadinali huagizwa kutotumia mwandiko wao wa kawaida. Iwapo hakuna kura ya uamuzi kufikia mwisho wa siku ya pili, siku ya tatu inatolewa kwa sala na kutafakari, bila kura yoyote kufanyika. Upigaji kura unaendelea kama kawaida baada ya siku hiyo. Mchakato wote unaweza kuchukua siku kadhaa au hata wiki.

Mara mbili kwa siku, kura huchomwa, na watu walio nje ya Vatikani huona moshi ukitoka kwenye bomba la Kanisa la Sistine.

Wino mweusi au mweupe huwekwa kwenye kura. Moshi mweusi unamaanisha kura bado haijaamua. Moshi mweupe unaonyesha Papa amepatikana.

Makardinali watapigia kura wagombea hadi jina moja litokee. Huku asilimia 80 ya Makadinali wakiteuliwa na Papa Francis, hii ni mara yao ya kwanza kumchagua Papa na watafanya hivyo kwa mtazamo mpana wa kimataifa.

Kwa mara ya kwanza katika historia, chini ya nusu ya Makadinali wapiga kura ndio wanatokea Ulaya. Brazil ina wawakilishi saba katika kundi hili.

 

Bunge la Ulaya Latoa wito wa Kuachiwa  kwa Lissu, Lasikitishwa na Tuhuma Zinazomkabili

Bunge la Ulaya Latoa wito wa Kuachiwa kwa Lissu, Lasikitishwa na Tuhuma Zinazomkabili

Wabunge wa Bunge la Ulaya wamejadili kwa dharura masuala ya kisiasa nchini Tanzania wakilenga kuhusu kesi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu na hatari ya hukumu yake iwapo atapatikana na hatia ya uhaini ambapo wametoa wito kwa Mamlaka za Tanzania kumuachia Lissu na kuweka mazingira rafiki kwa Vyama vya upinzani ikiwemo CHADEMA kushiriki uchaguzi wa mwaka huu 2025.

Bunge hilo limetoa wito kwa Serikali ya Tanzania kuirejesha CHADEMA katika mchakato wa kisiasa na kuhakikisha kwamba haki za Binadamu, uhuru wa kujieleza, na haki ya kupata haki Mahakamani na pia Serikali ya Tanzania imepewa wito wa kufuta adhabu ya kifo na kubadilisha hukumu zote za kifo.

Baada ya mjadala huo wa jana May 07,2025, Wabunge wa Ulaya wataandaa na kupiga kura juu ya azimio maalum lenye rejea 2025/2690 (RSP) leo May 8, 2025 kuhusu mjadala huo wa kesi ya Lissu ambapo Bunge hilo limetaka taarifa yao iwasilishwe kwa Serikali na Bunge la Tanzania, Umoja wa Afrika na Mwakilishi Mkuu wa Sera za Mambo ya Nje wa EU, kwa lengo la kuanzisha mashauriano ya dhati na yenye matokeo ya kweli kwa maendeleo ya kisiasa ya Tanzania.

Lissu anakabiliwa na mashtaka mawili ambapo moja ni la uchochezi na jingine ni la uhaini ambalo adhabu yake ni kunyongwa endapo atakutwa na hatia.

 

 

EU  Mbioni kusitisha Uagizaji wa gesi  Kutoka  Urusi

EU Mbioni kusitisha Uagizaji wa gesi Kutoka Urusi

Tume ya Ulaya imechapisha ramani inayoelezea mipango yake ya kukomesha utegemezi wa Ulaya kwa nishati ya Urusi katika miaka ijayo.

Chini ya mipango hiyo, uagizaji wa gesi yote ya Urusi na gesi asilia ya kimiminika kwa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya utapigwa marufuku kufikia mwisho wa  mwaka 2027.

Kujibu mipango hiyo, msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov aliliambia shirika la habari la Reuters siku ya Jumanne kwamba Ulaya ilikuwa ikijiwekea mazingira magumu yenyewe.

EU iliapa kusitisha uhusiano wake wa nishati na Urusi baada ya Moscow kuanzisha uvamizi wake nchini Ukraine mnamo 2022.

Vifungu vya mapendekezo ya kisheria vitawasilishwa mwezi Juni vikitaka nchi zote wanachama wa Umoja wa Ulaya kufanya mipango ya kitaifa ya kukomesha uagizaji wa gesi ya Urusi na mafuta ya nyuklia kulingana na Tume ya Ulaya.

Nchi wanachama wa EU lazima ziwasilishe mikakati chini ya mipango ya kuchukua nafasi ya uagizaji wa mafuta ya Urusi ifikapo mwisho wa 2027.

Nchi pia zimetakiwa kueleza mikakati ya kukomesha utegemezi wao kwa Urusi kwa madini ya urani urani iliyorutubishwa na vifaa vingine vya nyuklia.

Miji Muhimu Nchini Sudan yakosa Umeme baada ya kuripotiwa kwa Mashambulizi

Miji Muhimu Nchini Sudan yakosa Umeme baada ya kuripotiwa kwa Mashambulizi

Mashambulizi ya ndege zisizo na rubani yamepiga kituo kikubwa cha umeme katika mji wa Port Sudan nchini Sudan na kusababisha kukatika kabisa kwa umeme 

Milipuko na moto mkubwa umeripotiwa karibu na uwanja mkuu wa ndege wa kimataifa wa mji huo huku jeshi la wanamgambo likilenga mji huo muhimu kwa siku ya tatu mfululizo.

Safari za ndege zimekatishwa baada ya ndege zisizo na rubani kugonga uwanja wa ndege wa kimataifa na hoteli karibu na ikulu ya Rais huku Moshi mnene mweusi ukionekana alfajiri kwenye anga ya jiji ambalo hapo awali lilikuwa salama suala lililosababisha  maelfu ya watu wanaokimbia vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa miaka miwili wametafuta hifadhi.

Mapema hii leo  kampuni ya umeme ya Sudan ilisema  kuwa inatathmini uharibifu kwenye kituo chake, ambacho kimetatiza usambazaji wa maji, afya na huduma nyinginezo.

 

Visitor Counter

000969
Today: 14
Yesterday: 3
This Week: 17
Last Week: 49
This Month: 121

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz