CHADEMA Yalaani Uvamizi wa Makazi ya Viongozi Wao

CHADEMA Yalaani Uvamizi wa Makazi ya Viongozi Wao

Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA kimedai Jeshi la Polisi kuendesha operesheni haramu ya kuzingira na kuvamia makazi ya viongozi wa chama hicho ambao ni Mwenyekiti wa Chama Mh. Tundu Lissu na Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho. Mh. John Heche

Kwa mujibu wa Taarifa iliyo na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi Bi. Brandina Rupia imeeleza kuwa Katika makazi ya Mhe. Tundu Lissu, Askari wa Jeshi la Polisi wamevamia makazi ya Mh Lisu wakitaka kufanya upekuzi wa nyumba (upekuzi usiofuata sheria na taratibu), huku wakitumia lugha za vitisho na vitendo vinavyokiuka misingi ya kisheria na haki za binadamu.

Aidha taarifa hiyo imepinga kwa nguvu zote uvunjaji huo wa sheria na taratibu na kutaka majibu ya haraka kwa maswali sita waliouliza Jeshi la Polisi na Serikali ya CCM:

1. Kwa nini walitaka kufanya upekuzi usiku wa manane kama majambazi badala ya mchana kwa uwazi na kufuata taratibu na sheria?

2. Kwa nini hawakuonesha hati halali ya upekuzi kutoka mahakamani (Search Warrant) kama sheria inavyotaka?

3.Kwa nini hawakuambatana na kiongozi wa mtaa ili kushuhudia upekuzi kama taratibu na sheria zinavyowataka?

4. Kwa nini mnapanga kutekeleza au kufanya upekuzi katika nyumba ambayo mmiliki wake yupo gerezani na hawezi kushuhudia?

5. Je, Jeshi la Polisi linakusudia kumuweka Mhe. John Heche chini ya kifungo

GASCO kutumia Vifaa vya Kisasa Kuhakikisha usalama na Afya bora  kwa Wafanyakazi

GASCO kutumia Vifaa vya Kisasa Kuhakikisha usalama na Afya bora kwa Wafanyakazi

Kampuni ya Gesi Tanzania (GASCO) ambayo ni kampuni tanzu ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) imesema kuwa imewekeza vya kutosha katika matumizi ya teknolojia inayotumia akili mnemba (AI) kwa ajili ya kulinda usalama wa watu au wafanyakazi na mitambo ya kuchakata kusafirisha na usambazaji gesi asilia . 
 
Akizungumza wakati wa Maonesho ya Maadhimisho ya Wiki ya Usalama na Afya Mahala Pa Kazi Duniani yanayofanyika Kitaifa mkoani Singida, Afisa Usalama na Mazingira Mahala Pa Kazi wa GASCO Bw. Mlotwa Simbeye amesema kuwa shughuli za gesi asilia zinahitaji umakini mkubwa wa usalama na ndio maana wanatumia mifumo ya kisasa ya utambuzi na ung’amuzi wa vihatarishi mbalimbali kama vile gesi kuvuja au majanga ya moto ili kuzuia madhara yanayoweza kutokea.
 
Akiongea katika maonesho hayo, Mhandisi Hassan Temba amesema GASCO ina jukumu kubwa la usimamizi, uendeshaji na matenegezo ya mitambo ya Uchakataji, Usafirishaji na Usambazaji Gesi Asilia hapa nchini.
 
Pia, inahusika na ujenzi wa miundombinu ya gesi asilia ikiwemo ujenzi wa bomba la usambazaji wa gesi kwa wateja wa viwandani na majumbani pamoja na ujenzi wa vituo vya mafuta na gesi asilia kwenye magari (CNG)
 
“Ndio maana tumeamua kushiriki maonesho haya ili Watanzania waweze kujua kazi za GASCO kwa maendeleo ya nchi,” amesema Temba.
 
Aidha, Afisa Maendeleo ya jamii wa TPDC Bw.Oscar Mwakasege amesema kuwa TPDC ina majukumu mbalimbali ikiwemo kusimamia miradi ya kimkakati ya utafiti na utafutaji wa mafuta na gesi asilia nchini ukiwemo mradi wa utafiti wa mafuta Kitalu cha Eyasi Wembere ambao unagusa mikoa mitano (5) ikiwemo mkoa wa Singida (Wilaya ya Iramba na Mkalama).
 
‘‘Vilevile, TPDC ni mdau mkubwa wa maendeleo ya jamii kwani kupitia programu ya CSR miradi mbalimbali imetekelezwa ili kuleta ustawi wa na kudumisha mahusiano na jamii zinazopitiwa na miradi ya gesi asilia nchini. Mkoani Mtwara TPDC imekamilisha ujenzi wa kituo cha afya cha Msimbati mkoani Mtwara’’. Amesema Oscar
 
Kauli mbiu ya maonesho hayo yaliyoandaliwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) ni ‘Nafasi ya Akili Mnemba na Teknolojia za Kidijitali katika Kuimarisha Usalama na Afya Mahali pa Kazi’ ambapo mashirika na makampuni mbalimbali yameshiriki na kuonyesha mifumo yao ya afya na usalama kazini.
Dkt. Tulia Ackson  Awataka Wanachama wa CCM Kujiepusha na Makundi Ndani ya Chama

Dkt. Tulia Ackson Awataka Wanachama wa CCM Kujiepusha na Makundi Ndani ya Chama

Spika  wa Bunge na Rais wa 31 wa Muungano wa Mabunge Duniani IPU ,Dkt. Tulia Ackson, amewataka wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kibaha Mjini, mkoani Pwani, kuacha ushindani na makundi ndani ya chama  ambao unaweza kusababisha madhara kwa kutoa upenyo kwa upinzani wakati wa Uchaguzi. 
 
Akizungumza April 25, 2025 na viongozi mabalozi pamoja na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Jimbo la Kibaha Mjini, kutoka kata ya Viziwaziwa Kongowe na Msangani wakati wa uwasilishaji wa taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM, Dkt Tulia ambae alikuwa mgeni maalum aliongeza kuwa  waachane na ushindani ili kukiimarisha Chama.
 
"Msifanye ushindani wa namna ya Yanga na Simba, bali muangalie viongozi ambao wanaonekana kufanya kazi kwa manufaa yenu, wanaccm lazima tuwatupe mbali wapinzani, utekelezaji unaonekana kwa macho, Rais Samia Suluhu Hassan anastahili heshima kwa kumpa kura za ushindi na sio za kinyonge." alisema Dkt. Tulia
 
 
INEC Yatoa Vigezo Kwa Taasisi Za Kiraia Utoaji wa Elimu ya Mpiga Kura

INEC Yatoa Vigezo Kwa Taasisi Za Kiraia Utoaji wa Elimu ya Mpiga Kura

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetoa vigezo sita vya kuzingatiwa na taasisi za kiraia zinazotarajia kutoa elimu ya mpiga kura na uraia kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025.

INEC pia ilizitaka taasisi zinazotaka kutoa elimu ya mpiga kura na uraia kutuma maombi yao kuanzia jana Aprili 21, 2025 hadi Mei 20, 2025 ambapo taarifa ya Mkurugenzi wa Uchaguzi, Ramadhani Kailima ya Aprili 19, 2025 iliyotolewa jana ilieleza kuwa mwaliko huo umetolewa kwa kuzingatia kufungu cha 10 (1) (g) na (h) cha Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Namba 2 ya 2024.

“Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi katika kikao chake cha Aprili 3, 2025 imetoa mwaliko kwa taasisi na asasi za kiraia zenye nia ya kutoa elimu ya mpiga kura na uangalizi wakati wa uchaguzi wa Rais,Wabunge na Madiwani 2025,” alisema.

INEC ilibainisha vigezo hivyo ni taasisi na asasi kusajiliwa na sheria za Tanzania, taasisi na asasi hizo kufanya kazi kwa kipindi kisichopungua miezi sita tangu kusajiliwa kwake.

Pia, kwa taasisi zenye watendaji wa kimataifa, INEC ilisema ni lazima watendaji wawili wakuu kati ya watatu wawe raia wa Tanzania.

Tume ilieleza kuwa taasisi au asasi hizo hazipaswi kujihusisha na uchochezi au kuvuruga amani katika utendaji wake na zinatakiwa kuwa na uzoefu wa kutoa elimu ya mpigakura na iwe tayari kujigharamia katika kutoa Elimu ya Mpigakura.

Aidha, tume pia ilisema taasisi na asasi zitakazo tuma maombi ya uangalizi wa uchaguzi wanapaswa kuzingatia masharti yaliyopo kwenye mwongozo wa uchaguzi mkuu.

Asasi za kiraia na taasisi hizo zinapaswa kuainisha anuani ya taasisi au asasi zao, mahali taasisi au asasi husika inapofanyia kazi, shughuli zinazofanywa na taasisi au asasi husika kwa mujibu wa hati ya usajili.

Aidha, zinapaswa kuainisha mahali taasisi hizo inatarajia kwenda kuangalia uchaguzi huo, idadi, majina, na taarifa binafsi za watendaji wa taasisi au asasi zitawatumia katika usimamizi na uangalizi.

Pia, taasisi na asasi za kiraia zinatakiwa kuwasilisha majina na namba za simu  za viongozi wao.

Pia, asasi hizo zinatakiwa kuambatanisha nakala vivuli na nyaraka ya usajili wa taasisi au asasi husika na nakala kivuli ya Katiba ya taasisi au asasi husika.

Tume ilieleza maombi hayo yanapaswa kutumwa katika mfumo wa Kusajili Watazamaji, Asasi za Kiraia na Vyombo vya Habari na ilisisitiza kuwa maombi yatakayotumwa kwa njia tofauti na mfumo ulioainishwa hayatafanyiwa kazi.

Dkt. Mollel Afanya Ziara ya Kukagua Kituo cha Afya Cha Mama Ngoma

Dkt. Mollel Afanya Ziara ya Kukagua Kituo cha Afya Cha Mama Ngoma

Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel, amefanya ziara ya kukagua hatua zilizofikiwa katika utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu la kukipandisha hadhi Kituo cha Afya cha Mama Ngoma kuwa hospitali ya ngazi ya juu.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Dkt. Mollel amesema kuwa ameridhishwa na maendeleo yaliyofikiwa hadi sasa, na amesisitiza umuhimu wa mshikamano kati ya serikali na sekta binafsi katika kuboresha huduma kwa wananchi. “Tupo hapa kuhakikisha kilichoelekezwa na Waziri Mkuu kinatekelezwa kwa vitendo. Serikali haishindani na sekta binafsi bali tunashirikiana kutoa huduma bora kwa jamii,” amesema Dkt. Mollel.

Kwa upande wake, Profesa Ngoma ameishukuru Serikali kwa kutambua mchango wa kituo hicho katika jamii na kukipa kipaumbele. “Hili si jambo kwa ajili ya mtu mmoja, ni kwa manufaa ya wananchi wote wa eneo hili na maeneo ya jirani,” amesema Profesa huyo..

Uwepo wa Hospitali ya Mama Ngoma katika eneo la Kwangoa umetajwa kuwa muhimu kutokana na umbali wa hospitali ya wilaya, hivyo kusaidia kupunguza gharama za Serikali na kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi.

Visitor Counter

000960
Today: 5
Yesterday: 3
This Week: 8
Last Week: 49
This Month: 112

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz